Waswahili walisema ukistaajabu ya filauni utashangazwa na ya Musa, ama kweli wanadamu huwa hawakosi majina katika kila hali unayoipitia, ukiwa mwembamba watakuita kimbaumbau, na ukiwa mnene watakuita manyama uzembe, ili mradi tu wakupe kero na usijisikie furaha katika hali unayoipitia. Nimeanza na kuzungumza hayo kwasababu ya historia na shuhuda nzitto ninayotaka kuwaletea.
Leo nakwenda kumzungumzia Founder wa huduma ya Victory Faith, yenye makao makuu yake Arusha maeneo ya Kijenge Mwanama, anaejulikana kama Baba wa washindi Apostle Vincent Mkalla. Huyu ni mtumishi ambae Mungu anamtumia sana katika kufundisha mambo yanayohusiana na laana na jinsi ya kuziepuka.
Kwa mara ya kwanza nimesikia historia yake toka kwa wachungaji fulani ambao walimtambulisha kwangu kama Freemason mmoja hatari sana, na nilipotaka kujua ni kwa nini wanasema hivyo au ni kitu gani kinawapa uhakika kuwa huyu ni Freemason wengi walisema huyu ni mtumishi mwenye pesa na mafanikio makubwa sana na wao hawajui pesa hizo amezitoa wapi?? Hali hii ilinisababisha nimtafute mtumishi wa Mungu huyu na kutaka kujua kama kweli yeye ni freemason kama nilivyosikia ili nijue wanafanyajefanyaje huko kwa chama cha freemason?? Story niliyokutana nayo ni tofauti kidogo na ikanifanya nikae chini na kuwaletea ukweli wa mambo.
Huyu mtumishi ni mtoto wa kipekee wa kiume na wa mwisho kwa mzee Mkalla ambae alikufa wakati yeye akiwa na siku 22 tangu azaliwe.
Katika kukua kwake historia ya baba yake kufa na aligundua kuwa aliuwawa hali ile ilimjengea uchungu moyoni na akawa amepanga kuja kulipa kisasi kwa wale waliohusika katika kifo cha baba yake. Mbali na masomo aliyoyapata lakini piaa alitumia muda wake mwingi katika kufanya mazoezi na pia kujihusisha na michezo ya kung fu ambayo ilimuwezesha hadi kuvuka hadi boda za Tanzania na kwenda nchi mbalimbali kwa ajili ya mafunzo hayo, nchi kama vile urusi ambapo katika mchezo huo alifikia kiwango cha kutunukiwa mkanda mweusi. Hapo alikuwa ni mkristo lakini alikuwa hajaokoka na wala hajawa mtumishi bali alikuwa ni rastafari anaemiliki chuo cha karate alichokiita jina la scopion yaani nnge.
Miaka ilienda baadae akaja kuokoka, na siku alipookoka ndani ya siku mbili alinyoa rasta zake na kuendelea na kuwa mshirika mtiifu katika kanisa na pia muhudhuriaji na muhudumu katika mikutano ya injili.Na kazi yake kubwa ilikuwa ni kusafisha vyoo vya kanisa na kuhakikisha ni visafi kila wakati, kazi hiyo haikuwa na malipo ilikuwa ni kazi yake ya kujitolea na baadhi ya waumini wa kanisani wakambatiza kwa jina la kebehi la bwana mavi. Mwaka 1996 akiwa tayari ameshakomaa kwenye wokovu ndio mwaka aliofunga safari kutoka moshi na kuingia katika jiji la Arusha akiwa kamamgeni, ambapo moja kwa moja akaenda kufanya kazi ya umisionary katika kijiji kimoja cha Kimnyaki huko Meru. Huko aliweza kukutana na watumishi wa Mungu mbalimbali wakiwemo akina Askofu Ngataiti na Askofu Lyzer wa kanisa la habari maalum ambao hivi sasa ni marehemu.
Wakati huo Apostle Vincent Mkalla hakuwa ameoa, na alikuwa ni miongoni mwa watumishi maskini sana, ambapo alikuwa amepewa hifadhi katika nyumba moja ya udongo ajihifadhi kama mtumishi, na humo ndani ya nyumba hakuwa na kitanda wala godoro bali alikuwa amemwaga mchanga mwingi chini, na ametengeneza mbao kama ile chaga, na juu ya hizo mbao ndio alikuwa analala, huku shuka yake ikiwa ni ile mifuko ya visalfeti ambayo huwa anakuja huku tz ikiwa imebeba viatu vya mitumba na mto wake ulikuwa ni biblia. Mwaka 1997 watumishi walikaa chini na kukubaliana kupinga tohara za jadi kwa wamasai baada ya kugundua wale wamasai wenye asili ya kiarusha tohara zao huwa zinaambatana na mambo mabaya ambayo ni ibada za mizimu, kwa mfano kila tohara ya hao wamasai wa asili ya kiarusha kabla ya kutahiri vijana huwa wanamuita Laibon ambae ni mganga wa kienyeji anaekwenda kwenye milima ya meru na kufukua jiwe fulani kila baada ya miaka saba na kuweka wakfu tohara hiyo huku wakiwa wanaimba nyimbo zao. Na kuna mengine mengi mabaya ambayo watumishi wa Mungu waliyabaini na kuamua kupinga tohara hiyo ambapo baadhi ya vijana wa kimasai waliafiki kutoshiriki tohara hiyo na kutaka watairiwe lakini bila muongozo wa mganga wa kienyeji Laibon, wala pasipo kuimbiwa nyimbo za kiasiri. Apostle Vincent Mkalla na mzee wake wa kanisa anaejulikana kama Ayubu ambae hivi sasa ni Mchungaji waliafiki kuwatahiri vijana hao kama walivyodai, hivyo wakachukua pesa kama shilingi laki nne kasoro na kuanza safari ya usiku kwenda kijiji cha jirani ili kuwatahiri vijana hao, wakati huo alikuwa katika mfungo wa siku 62, njiani walikutana na majambazi ambapo vijana pamoja na mchungaji Ayubu walikimbia lakini kwasababu yeye alikuwa kwenye mfungo alijikuta anaanguka chini na wale majambazi wakamkamata na kumuwekea bunduki kichwani huku wakimlazimisha atoe hela, akiwa katika kuwasikiliza jinsi alivyokuwa mchovu kwa ajili ya mfungo na koti alilovaa alisikika jambazi mmoja akisema "Achana nae huyu mzee atakuwa hana hela" na hiyo ndiyo ikawa pona yake. Alipoamka hapo aliendelea na safari ambapo mbele ndipo alikutana tena na mzee wa kanisa pamoja na wale vijana ambao walikimbia, safari yao ya kwenda kwangariba ikaendelea. walifanikiwa kufika kwa ngariba mida ya saa saba usiku na kazi ya kutahiri wale vijana ikaendelea, maana vijana walikataa kutahiriwa kimira lakini vilevile walikataa kutahiriwa kwa ganzi. Baada ya tohara hiyo walirudi kijiji cha Kimyaki ili wawarudishe kila kijana nyumbani kwao kabla ya wazee wamji kugundua kama vijana hawajatahiriwa kimira. Wakati wanarudi walifika kwenye daraja moja ambapo vijana walishindwa kuvuka ikabidi Apostle Vincent na Mchungaji Ayubu waanze kumvusha mmoja baada ya mwingine katika daraja lile, jambo la kushangaza nyuki waliwavamia na kuanza kuwang'ata kwelikweli lakini Mungu akawasaidia wakavuka salama, na mida ya saa kumi kuelekea kumi na moja walifanikiwa kufika kijijini na kumrudisha kila kijana nyumbani kwao. Baada ya wiki moja tukio lile likavuja lakini haikujulikana moja kwa moja ni nani aliyewapeleka vijana wale kwenye tohara, maana katika tohara wamasai wanakuwaga na mtu anaeitwa mdhamini, yaani mtu anaemshikilia kijana wakati wa kutahiriwa, sasa vijana wale walikamatwa na kuanza kuteswa huku wakiulizwa ni nani alikuwa mdhamini wake lakini wao wakajibu kuwa waliegamia mti, ambapo gadhabu ya wamasai wale waliielekezea kwenye mti walioelekezwa na wakaenda kuung'oa. lakini baada ya mti walianza operation ya kushughulika na wachungaji, ambapo jumanne moja Apostle Vincent alikuwa kanisani akiwa ametangaza semina, alishangaa amevamia na watu zaidi ya mia saba pale kanisani ambapo walimpiga fimbo za kutosha na wakamvunja mguu, na kuna bibi mmoja aliyekuwa muumini katika kanisa hapo alipigwa fimbo hadi akafa. Tukio hilo lilikuwa baya sana kiasi kwamba wachungaji wengine ambao walikuwa ni wenyeji wa jamii ile walikimbia na kuacha makanisa yao, wengine walikimbilia Kenya, wengine Morogoro, wengine Dodoma, huku wengi wakidhania Apostle Vincent amefariki dunia. Na kumbe Mungu alimponya na shambulizi lile lakini habari zilifika hadi kwa mama yake kuwa ameshafariki. Baada ya tukio hilo alitibiwa na akafungwa pop na akaendelea kusimama kwenye semina huku akiwa na muogo mguuni. Yeye aliendelea kumtumikia Mungu katika eneo lile ambapo jambo hilo lilisababisha hata wamasai wa jamii ile wamuhesabu kama mchungaji shujaa. Na habari hiyo ilivuma hadi kutangazwa kwenye vyombo vya habari kama vile bbc na sauti ya ujermani, hivyo ikaleta promo ya kiaina pale kijijini na kufanya semina ipete mahudhurio makubwa. Mwaka 1998 Apostle Mkalla alipata mchumba na mwaka 1999 akaoa, baada ya kuoa alikuwa amezawadiwa vyombo vya ndani na na mazagazaga kibao kama mnavyojua mambo ya harusi, lakini Mungu akamwambia jambo na akamshirikisha mke wake wakakubaliana kuchukua vitu vyao vyote na kwenda kumbariki Mchungaji mmoja ambae alikuwa anapitia katika wakati mgumu na hakuwa na vyombo vya ndani, na wao wakabakia hawana chochote kisha wakaanza kumlilia Mungu. Kweli walipita katika wakati mgumu sana wa kukosa hadi chakula lakini walidumu katika kumuamini Mungu. Baada ya muda ndio Mungu akaanza kumfungulia milango ya kihuduma na kifedha, akafunguliwa mlango wa kufaa sana katika nchi za jirani kama Kenya na UGANDA ambapo katika mikutano yake Mungu alimuinulia watu wa kusuport. Sasa wale wachungaji waliokimbia vita vya tohara baada ya kurudi na kukuta mwenzao alivumilia mateso na hakumkana Yesu wala kuiacha kazi yake ndio wlianza kuleta uvumi na maneno ya kumchafua. Zikaandikwa bbarua zikapigwa sahihi za wachungaji, zikasambazwa makanisa mengi ya Arusha kwmba huyu ndugu ni freemason, anakunywa damu za watu katika kila ajali inayotokea Arusha, wengine wakavuka hadi Kenya na kuongea kuwa akija Kenya anakuwa anaambukiza dhambi kwasababu ana watoto wengi mitaani na ameoa wake mengi, lakini hayo yote hakuyajibu bali alimkabidhi Mungu na Mungu akamjibia. Bado Mungu aliendelea kumfunguliamilango ya nnje ya nchi na kumpa kibari katika nchi kama vile SUDAN na Somalia ambapo amefungua huduma kadhaa huko. Mbali na huduma pia ni mfanya biashara, na mfugaji, na pia ana mashamba yake pamoja na nyumba kadhaa za kifahari. Ila siri ya kupata vyote hivyo ni utoaji, anaamini sana katikakutoa na pia katika kuwaheshimu masihi wa Bwana. Kwa hiyo toka katika jina la bwana mavi enzi hizo akiwa amepigika lakini leo anaitwa Freemason baada ya Mungu kumbariki. Ama kweli kila hatua unayoipiga maishani huwa inaambatana na majina yake. Sasa na mimi nimegundua kuwa hata kutukanwa na kuzushiwa pia ni sehemu ya baraka.
Tarehe 22/23 Agosti 2015 Apostle Mkalla ambae ni mlezi wa Makamanda wa Yesu atasimama pale Landmark Hotel na kufundisha siri ya kufanikiwa, pamoja na uvumilivu wa kuwashinda waswahili na maneno yao.
No comments:
Post a Comment