Tuesday, June 9, 2015

SIKU MBILI ZA MAKAMANDA NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM ZINAZIDI KUVUMA NA KUTIKISA AKILI ZA WENGI

Semina ya siku mbili inayotazamiwa kufanyika tarehe 22 hadi 23 Agost 2015 katika Ukumbi wa LandMark Hotel, Dar es salaam, Ni semina ambayo awali ilijulikana kama semina ya From receiving to giving lakini kwa sasa imebadirika na kuwa semina ya Growing Without Groaning in Life &Ministry. Ni semina ambayo watumishi wanne watasimama kwenye madhabahu moja katika nyakati tofauti tofauti, Wanenaji katika semina hiyo ni Founder wa huduma ya Victory Faith Tanzania Apostle Vincent Mkalla toka Arusha, Mtume Wa Urejesho Peter Nyaga tokea RGC Miracle Centre Tabata  Chang'ombe, Apostle Livingstone Banjagala wa Citty Harvest International Church Dar Es Salaam, Pamoja na Mwalimu Steven Haule country Manager wa Letshego Tanzania Limited na pia MD wa Chama cha kusaidiana cha wafanyakazi wa Tegeta,  hawa wote ni waalimu wazuri sana katika maisha na mambo ya kiroho pia hivyo natarajia mabadiriko makubwa sana kwa wale watakaohudhuria katika semina hii. Waimbaji watakaohudumu katika semina hii ni Tumaini Njole, Kuyokwa Mary, Veejay Shwarikuu, King David, Stella Swai, Elandre, Baba Sam, Gastor Sapula, Kuhani Zangina, na wengine wengii. Praise and worship itaongozwa na Bishop Nickodemus Shaboka Jr pamoja na team yake. Hii sio ya kukosa maana watumishi wengi watakuwepo katika semina hii..

No comments:

Post a Comment