Thursday, June 11, 2015

MTUME WA UREJESHO PETER NYAGA ATOA SHILINGI LAKI SABA KAMA SUPORT YAKE KATIKA SEMINA YA MAKAMANDA

Katika semina ya siku mbili ya makamanda wa Yesu inayotazamiwa kufanyika  tarehe 22 hadi 23 Agosti 2015 katika ukumbi wa Landmark Hotel uliopo Ubungo, Riverside, mambo yanaendelea kuwa mazuri. Katika semina hiyo iliyopewa title ya "GROWING WITHOUT GROANING IN LIFE AND MINISTRY" ambayo itawakutanisha waalimu wazuri na wenye viwango vya hali ya juu kwenye maisha na kihuduma kama vile Baba wa washindi Apostle Vincent Mkalla tokea Arusha, Apostle Livingstone Banjagala,  Mtume wa Urejesho Peter Nyaga, pamoja na mwalimu Stephen Haule, mbali na kuwa mmoja miongoni mwa waalimu lakini Mtume Nyaga ameamua kupanda mbegu yake na kudhamini semina hiyo kwa kutengeneza matangazo yenye gharama ya shilingi laki saba za kitanzania. Kwa niaba ya makamanda wa Yesu, General Comandoo Mtume Kijana Bashando ametoa shukrani zake za dhati kwa Mtume wa urejesho Peter Nyaga kwa kujitoa kwake. Lakini pia amewashukuru waalimu wote waliokubali kushiriki katika semina hiyo na kufundisha watanzania watakaobahatika kuhudhuria kwenye semina hiyo. "Mungu ambariki sana Peter Nyaga na wengine wote wanaotoa suport kwa ajili ya kuwezesha siku hizi muhimu sana ambazo naamini zitakwenda kuwabadirisha watu wengi" alisema Bashando. Kama una biashara au kampuni na ungependa na wewe kuwa mdhaminimmoja wapo katika semina hii unaweza kuwasiliana nasi kupitia simu namba +255713700627l, +255763788459 au kwa email bashandomarwa@gmail.com

1 comment: