Saturday, January 28, 2017

BAADA YA UKIMYA MREFU PETER BANZI AAHIDI KURUDI KWA KISHINDO

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili Peter Banzi baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu ameamua kuibuka na kusema kuwa alikuwa anatafuta utulivu ili awe karibu zaidi na Mungu. Mtumishi wa Mungu Peter Banzi ambaye alitamba kwa kibao chake Utukufu wako Baba chukua, Upako download na vingine vingi, amesema hivi sasa amerudi akiwa sio muimbaji pekee bali ni muhubili wa injili.

Peter Banzi ambae ana huduma yake ya kuwahubilia vijana wa mitaani pamoja wale walioathiliwa na madawa ya kulevya amesema kuwa wito wake sio kuimba tu bali ni kuwafikia walioko gizani na kuwafikishia nuru ya Kristo. Itakuwa haina maana nije kanisani jumapili na kuimba nikashangiliwa na kuuza cd tu wakati kuna wana kitaani wamepoteza, na hakuna wa kuwaondoa katika shimo walilodumbukia, alisema Peter Banzi. 

Mbali na yote hayo Peter Banzi ni mume na baba wa mtoto mmoja, hivyo anasema muziki wake inabidi aufanye kiutu uzima zaidi.

Sisi kama Makamanda, tunamtakia kila la kheri Mtumishi Peter Banzi.


No comments:

Post a Comment